Wednesday, March 14, 2012

Onemocke

Airtel yaja na internet ya 3.75G kutoa ubora na kasi zaidi kwa wateja.

Meneja Masoko wa Airtel Bw Salim Madati akitoa ufafanuzi kwa waandishi
wa habari juu ya huduma mpya ya 3.75G katikati uzinduzi uliofanyika
leo katika makao makuu ya Airtel Morocco ambapo sasa wateja wa Airtel
wataweza kupata huduma ya internet iliyo ya kasi na kuwapatia ufanisi
Zaidi katika shughuli zao za kila siku.
Airtel Marketing manager Salim Madati explicate on 3.75G data service
to the press during the launch of 3.75G mobile platform in the
country, which promises to change how subscribers experience the web
on internet-enabled cell phones. The launch ceremony held at Airtel
headquarter Morocco and attended by members of press


Mkurugenzi mkuu wa Airtel Bw Sam Elangallor akionyesha jinsi gani
huduma ya 3.75 inavyoweza kutoa huduma ya internet iliyo ya kasi na
kuwawezesha wateja wa Airtel kufanya video call wakati wa  uzinduzi wa
huduma ya 3.75 iliyofanyika makao makuu ya Airtel na kuhudhuriwa na
waandishi wa habari , wakishuhudia (kulia) ni mkurungezi wa
mawasiliano wa Airtel Bi Beatrice Singano Mallya na (kushoto )ni
Meneja masoko Salim Madati.
Airtel Managing Director Sam Elangalloor reveal 3.75G technology which
will enhance multimedia functionality, high speed mobile broadband and
internet access; allowing  Airtel Customers  to make video calls,
watch live TV, send and receive emails, and download music from the
handheld devices. During 3.75G  launch ceremony held at Airtel
Headquarters and attended by media on the (left) Airtel communication

Director Beatrice Singano Mallya and Marketing Manager Salim Madati

Mkurugenzi mkuu wa Airtel Bw Sam Elangallor akiongea na waandishi wa
habari (hawapo pichani) wakati wa halfa fupi ya  uzinduzi wa huduma ya
3.75G  ambayo itatoa huduma ya internet yenye ubora na kasi zaidi  kwa
watumiaji wenye simu zenye uwezo wa kutumia internet wawapo mahali
popote. Uzinduzi huu ulifanyika katika makao makuu ya Airtel morocco
Airtel Managing Director Sam Elangalloor reveal 3.75G address the
member of press (not in picture) during the 3.75G service that will
provide high speed mobile broadband and internet access and allowing

Airtel customer use fast internet service anywhere in the country.

Mkurugenzi mkuu wa Airtel Bw Sam Elangallor na mkurungezi wa
mawasiliano wa Airtel Bi Beatrice Singano Mallya  kwa pamoja
wakionyesha jinsi gani huduma ya 3.75G  ilinavyoweza kuwawezesha
wateja wa Airtel kupata huduma ya internet yenye ubora na kasi zaidi
kwa watumiaji wenye simu zenye uwezo wa kutumia internet ikiwa ni
pamoja na  kufanya video call wakati wa halfa fupi ya uzinduzi wa
3.75G  iliyofanyika makao makuu ya Airtel Morocco.
Airtel Managing Director Sam Elangalloor and Airtel communication
Director Beatrice Singano Mallya jointly demonstrate how 3.75G
capability will allow Airtel customers to make video calls, watch live
TV, send and receive emails and download music from their cellular
phones, this occurred  during the launch held at Airtel Headquarters

Morocco 

Mkurugenzi wa Airtel Sam Elangallor akiinua modem na kumkabidhi
Mwandishi wa habari kutoka TBC Jane John aliyejishindia modem wakati
wa uzinduzi wa huduma ya 3.75G iliyofanyika makao makuu ya Airtel na
kuhudhuriwa na waandishi wa habari, wakishuhudia ni baadhi ya
wafanyakazi wa Airtel
Airtel Managing Director Sam Elangalloor handover a modem to TBC news
reporter Jane John who won herself a modem during  Airtel 3.75G launch
ceremony held at Airtel headquarters and attended by members of press,
in the picture are Airtel staff  representatives 

Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Bi Beatrice Singano Mallya akiongea
wakati wa uzinduzi wa huduma ya 3.75G uliofanyika leo katika makao
makuu ya Airtel Morocco ambapo sasa wateja wa Airtel watapata internet
yenye ubora na kasi  zaidi  , Pichani ni Mkurugenzi wa Airtel Sam
Elangallor

Airtel yaja na internet ya 3.75G kutoa ubora na kasi zaidi kwa wateja.
•    Airtel yajenga mtandao bora wa data barani Afrika
•    Uzinduzi wa Airtel 3.75G Tanzania utawapatia watumiaji  wa data
huduma yenye kasi na ubora zaidi  katika simu zao
•    Kupitia internet ya 3.75 itawawezesha wateja kufanya maongezi ya
simu ukiwa unamwona mtu, kuangalia TV, kutuma na kupokea barua pepe na
kuperuzi na kupata miziki kutoka kwenye tovuti kupitia simu zao.
Jumanne 13 Machi 2011, Dar es Saalam–Airtel Tanzania leo imepiga hatua
kubwa katika kujenga na kukuza mtandao wa technoloijia ya 3.75G Africa
kwa  kuzindua rasmi  mtambo wa 3.75G nchini Tanzania,ambapo Airtel
itatoa huduma ya internet yenye ubora na kasi zaidi  kwa watumiaji
wenye simu zenye uwezo wa kutumia internet wawapo mahali popote.
Mkurungenzi Mkuu wa Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Sam
Elangalloor alieleza” kukua kwa technolojia hii kutakuza ufanisi
katika vyombo mbalimbali vya  mawasiliano (multimedia), kwa kuwa 3.75G
itatoa internet yenye ubora na kasi  zaidi kwa  kuwezesha wateja
kufungua tovuti mbalimbali, kufanya maongezi  ya simu kwa njia ya
video , kuangalia TV, kutuma na kupokea barua pepe na pia  kupata
muziki kutoka kwenye tovuti  kwa kutumia simu
Teknologia ya 3.75G itatoa nafasi kwa wateja kupata mawasiliano ya
data kwa njia tofauti na ya pekee kabisa, ndio maana leo Airtel
tunajisikia fahari kuwa internet yetu ya 3.75G ni uvumbuzi na
muendelezo wa mtandao (platform) wetu ili kuwawezesha wateja wa Airtel
wote nchini kupata huduma ya internet au data yenye ubora wa hali ya
juu pamoja na kasi zaidi”
Tunafanya ubunifu wa kuleta huduma zenye ubora zaidi katika mtandao
kwa kuzingatia kuwa sasaivi dunia inauhitaji mkubwa sana wa huduma za
kimtandao hasa kupitia simu ya mkononi
Ukirejea takwimu zilizofanywa na kampuni ya McKinsey & Co.
Telecommunications zinaonyesha  mpaka sasa kuna watumiaji wa simu za
mkononi wapatao milioni 400 Afrika, na kwamba bara la  Afrika ni moja
kati ya  soko linalokuwa kwa kasi zaidi huku soko la simu za mkononi
likiendelea kukua na kupanuka zaidi na kufikia kutoa huduma za
internet, huduma za benki kwa njia simu (mobile banking)  na biashara
kwa njia ya mtandao yaani (mobile commerce) .

Hivyo basi kwa kuzingatia hili,  ndio maana Airtel tunaendelea na
mikakati kama hii ya kuwaletea wateja internet yenye kasi zaidi ya
3.75G ambayo ni sambamba  na lengo letu la kuendea kupanua mtandao
ili kutoa mwanya wa mawasiliano kuwafikia wakazi wengi wa vijijini
ambao walikuwa wamesahaulika na mapinduzi ya mawasiliano katika bara
la Afrika.
“wote tunafahamu kuwa mawasiliano ni nyenzo muhimu kwa maendeleo ya
jamii ya sasa lakini bado kunachangamoto kubwa sana katika kupata
huduma hii kwa baadhi ya sehemu barani Africa. Lakini tukumbuke
Mawasiliano ni haki ya msingi kwa kila mtu na si vinginevyo hivyo kwa
kupitia mtandao wa Airtel internet yenye kasi zaidi ya 3.75G ninaamini
tutaweza  kuunganisha idadi kubwa ya watu kwa kukuza mahusiano ndani
na nje ya ya jamii zetu, kuendeleza na kuutangaza utamaduni wetu,
pamoja na kupanua wigo wa wale wanaofanya biashara kupitia mtandao wa
internet “ Aliongeza Elangalloor.
Ikiwa tayari mteja ameunganishwa na teknologia ya 3.75G simu yake
itaonyesha 3.75G, HSDPA, WCDMA or HSPA. Hii inategemeana  na Aina ya
simu aliyonayo mtumiaji lakini kasi ya kuunganishwa ni yenye ubora
zaidi.
Airtel itaendelea kuwekeza kwenye huduma ya data katika soko lake lote
huku lengo likiwa ni kuwa mtandao mpana zaidi wa teknologia ya 3.75G
katika bara zima, na itaendelea kutoa huduma bora na inayokidhi
mahitaji ya watumiaji

- Ends-

OneMocke

blogspot.com">oB3c.blogger">ASRock X79 Overclock ‘KING' MotherboardbrBroke 3DMark 11 World Record!

I would be killed very resourceful in my imagination

Sunday, March 11, 2012

MASHINE YA KUINUA MATITI YA WANAWAKE YAINGIA TANZANIA


BIASHARA huria imezua mengi. Hali kadhalika Sayansi na Tekenolojia nayo, imeleta mengi. Katika kuwaondolea kero  wanawake wenye matiti yaliyosinyaa hapa nchini, wataalamu kutoka China wameanza kutoa huduma ya kunyanyua matiti hayo kwa kutumia mashine maalumu.

Wachina wamejipatia umaarufu katika kuleta bidhaa mbalimbali hapa nchini, zikiwamo za kuongeza nguvu za kiume, kupunguza uzito, kuotesha nywele, kujichubua (kumfanya mtu mweusi awe mweupe), kuongeza makalio nk.

Huduma hiyo ya kusimamisha matiti yaliyolala, imeanza kutolewa katika Saluni ya Blue Palace, iliyopo nyuma ya Shule ya Mapambano, Sinza jijini Dar es Salaam.

Haikuwa rahisi kuweza kuamini kuwa vitu kama hivi vinaweza kupatikana Tanzania. Mwananchi Jumapili lilifunga safari mpaka kwenye saluni hiyo inayomilikiwa na Sarafina Mtweve, kujionea jinsi teknolojia hiyo inavyofanya kazi.
Mbali na meneja wa saluni hiyo, Trust Mwembe, pia alikuwepo mtaalamu kutoka China aitwaye, Ciisy Pang, ni binti wa miaka 23 tu, lakini anasema kwa miaka minne amefanya kazi hiyo na kuwasaidia wanawake mbalimbali waliokuwa wakikerwa na matiti yaliyolegea au kuanguka.

Pang na kundi lake wanatoa huduma hii kwa gharama ya Sh150,000 kwa kuanzia, ingawa wanahisi gharama hizo zitapanda katika siku chache zijazo.

 Jinsi matiti yanavyosimamishwa
Mashine hiyo inayoitwa ‘Beauty Machine’ ina uwezo wa kusimamisha matiti ya kila saizi kwa kuwa huambatanishwa na vibakuli (cups) kama unavyoona pichani.

Kazi kubwa ya mashine hiyo ni kuamsha misuli ambayo hushikilia nyama za matiti.
Pang anasema, zoezi la kusimamisha matiti huchukua wiki tatu mpaka sita, inategemea aina ya mteja na wakati mwingine juhudi zake.

Mtaalamu huyo ambaye anazungumza Kichina na kutafsiriwa na meneja wa saluni hiyo, anaelezea namna anavyofanya kazi ya kuyarudisha matiti  kwa muda huo.

 “Kwanza unapaswa ujue kuwa hatutumii dawa yoyote katika zoezi hili, mteja wetu akifika hapa, kinachotumika ni mashine tu ambayo hutumia umeme kama zilivyo dryer  za nywele,
“Baada ya kumlaza katika kitanda kile, tunachukua kitu mfano wa bakuli (cups) mbili kulingana na ukubwa wa matiti yake, tunayatumbukiza humo, kisha tunawasha mashine,” anasema Pang.

Mtaalamu huyo anasema mashine hiyo ikiwashwa  inavuta kama ‘vacuum’, na inaweza kuongezwa kasi au kupunguzwa kama inavyofanyika kwenye mashine za kufanyia mazoezi.

“Tunaiwasha mashine kwa muda wa dakika 45, mteja atachagua siku mbili katika wiki za kufanya zoezi hili mpaka litakapokamilika,”anasema Pang.

Tangu mashine hiyo iwasili nchini, takribani mwezi mmoja uliopita, Pang anasema ana wateja wanane anaowahudumia kwa nyakati tofauti ambao wamekiri kuwa maendeleo yanatia moyo.

 Ni kweli mashine hii inasaidia?
 Akizungumza kwa njia ya simu, mmoja wa wateja anayepata huduma hiyo ambaye alijitambulisha kwa jina moja tu Irene anasema, ni wiki ya tatu sasa tangu aanze kupata huduma hiyo, anakiri kuwa matiti yake sasa yameanza kuwa magumu tofauti na mwanzo.

 “Kusema kweli nilikuwa na matiti yaliyosinyaa wala si kulala tu kama ulivyouliza, ila naona sasa yameanza kuwa magumu na kurudi juu kidogo,” anasema Irene.

 Akizungumzia ugumu anaoupata katika zoezi hilo, anasema safari za kila wiki saluni na zile dakika 45 za kukaa kwenye mashine zinamchosha, lakini kwa kuwa amedhamiria, amejitoa mpaka zoezi hilo litakapokamilika.
Matiti yanaweza kulegea tena?

Pang anasema kama matiti yanalegea kwa sababu fulani mfano uzazi wa watoto wengi, basi yanaweza kulegea tena kama mtu atajifungua na kunyonyesha kwa muda huo.Aidha anasema wanawake wenye matiti makubwa, ni rahisi kuanguka kama hawatayavalisha sidiria kwa muda mrefu.

 “Wanawake wenye matiti makubwa huwa nawashauri kuvaa sidiria hasa wakati wa mchana na usiku wanaweza kuacha kuzivaa, hii inasaidia kuimarisha misuli inayoyabeba matiti,” anasema Pang.

 Jamii inazungumziaje jambo hili
Baada ya kusikia kuwepo kwa mashine hii nchini, wanawake mbalimbali wamesema wanatamani kupata huduma hiyo lakini wengine, walionyesha woga juu ya matokeo yake.

 “Ni kweli baada ya kunyonyesha watoto wawili sasa matiti yamelegea kabisa, natamani yarudi kama wakati ule wa usichana wangu, lakini nahofia huenda mbele ya safari nikapata madhara,” anasema Linda Masatu.

Linda anaongeza kusema kuwa ni vizuri mwanamke akawa na matiti yaliyojaa vizuri, lakini anahofia njia zinaweza kuwa na madhara, huku akisema kama ingetokea njia nyingine ya asili asingesita kuifuata.

Naye Batuli Famau, anasema mwanamke anapokuwa na matiti yaliyosinyaa mvuto wake hupungua, hata anapovaa sidiria anakuwa amebadili mwonekano wa nje tu, lakini ndani bado anakuwa vilevile.

“Mwanamke mrembo ni yule mwenye matiti mazuri, sasa inapobidi kutumia njia fulani ili yarudi kama tulipokuwa vigoli, tutafanya tu ili mradi kama njia hizo hazitatuangamiza,” anasema
Wanaume nao wameonekana kuunga mkono zoezi la kusimamisha matiti ingawa wengine hawaungi mkono utumiaji wa mashine hii.

Augustino Magara anasema: “Ni kweli mwanamke mwenye matiti magumu anavutia kuliko yaliolegea na kulala, lakini sasa tuwe makini kabla wake zetu hawajaumia katika mashine, hizi”

“Wote tunajua sababu zilizosababisha matiti ya wake zetu yalegee, sioni sababu ya kusema tunataka yaliyomagumu, tuwapende wake zetu hivi hivi na tuwape moyo,” anasema Nganara.

Dk Innocent Mosha wa Kitengo cha Patholojia Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, anasema ni vigumu kwa wataalamu wa afya kugundua madhara ya mashine hizo kwa haraka hadi pale uchunguzi utakapofanyika.

“Ingelikuwa mazoezi hayo yanachukua muda mfupi, kweli tungepata wasiwasi kwa kuwa, unapoisimamisha misuli kwa haraka ni lazima madhara yatokee, lakini hili la mazoezi, bado sifahamu,” anasema  Dk Mosha.

NIKITAPA SHOO NYINGI KUCHEZA FILAMU NITASIMAMA KWA MUDA – SHILOLE…!!


MSANII wa filamu ambaye kwa sasa amejikita zaidi kwenye muziki, Shilole (mkali wa mauno), amedai kuwa endapo kama atapata kazi nyingi za kufanya shoo anaweza kuachana na filamu kwa muda kwani tayari mashabiki wengi wameanza kujitokeza katika shoo  zake.

Hayo aliyasema wakati akizungumza na Dartalk, juu ya maisha yake ya sanaa pamoja na mpangilio wake wa muda kwani kwa sasa anaonekana zaidi kwenye matamasha ya muziki kuliko filamu.

Alisema yupo mjini kwa lengo la kutafuta pesa hivyo endapo atakuwa bize na shoo za muziki anaweza kusimama kwa muda kufanya filamu kwani kila kitu kinaenda kwa ratiba.

“Endapo nitakuwa bize sana na muziki naweza kusisima kwa muda kucheza filamu, kwa sababu kila kitu kinaenda kwa ratiba lakini hata hivyo siyo kwamba kwa sasa sifanyi filamu kazi ipo palepale,” aliema.

Aliongeza kuwa fani ya muziki imeweza kumtoa katika maisha fulani na kumpeleka hatua nyingine ambayo anamshukuru mungu kwani anaamini baada ya miaka kadhaa mbele anatakuwa mbali zaidi.

“SHETTA” ATAMANI KUFANYA KAZI NA WASANII WA ‘YMCMB’…!!


MSANII wa muziki wa kizazi kipya bongo, Shetta, amedai kuwa anapenda siku moja aje kufanya kazi na wasanii wa kundi la  ‘YMCMB’ kutoka Marekani, kama vile Lil wayne, Birdman, Nicki Minaj na wengine.

Shetta alitoa kauli hiyo baada ya Onemocke kutaka kujua ni kundi gani la muziki la Marekani ambalo analizimia sana kutokana na kazi zao pamoja maisha ya yao ya utajili.

Ambapo alisema kuwa wasanii hao wanauwezo mkubwa katika kuimba ingawa wapo wengine anaowazima, lakini kwa wasanii wa kundi hilo anaamini ipo siku atakuja kufanya nao kazi.

Aliongeza kuwa anajua kwa sasa hawezi kukutana nao lakini kutokana na juhudi anazozifanya anaamini siku moja milango itafunguka na ataweza kukutana nao.

“Wapo wasanii wengi ambao napenda kazi zao pamoja na maisha yao, lakini kundi hilo ni kati ya yale ambayo yapo ndani ya damu na kikubwa ambacho nawaza kila siku ni ile siku ambayo nitakuja kufanya nao kazi hata moja tu,” alisema.

“REHEMA FABIAN” AFIKIRIA KUACHANA NA SANAA…!!


MSANII wa filamu bongo Rehema Fabian, baada ya kutaka kunywa sumu kwa lengo la kujiua, sasa amefunguka na kudai kuwa anafikilia kujitoa kwenye kila kitu kinachohusiana na sanaa kwani anahitaji kufanya ishu zake mwenyewe.

Fabian alizungumza na mtandao wa OneMOcke na kueleza ishu hiyo kwani anaamini ndiyo iliyosababisha hadi kufikia hatua ya kutaka kutoa uhai wake.

Alisema kuwa hata hivyo bado anafikilia juu ya ishu hiyo kwani ni hatua ambayo anahitaji kumshiriki mtu ili aweze kumpa ushauri pamoja kuchangua kazi nyingine anayoweza kufanya.

“Nafikilia kuachana na mambo yote yanayohusu sanaa kwa sababu nashindwa kufanya mambo yangu ya maana kwa kuogopa watu hivyo naweza kujihusisha na biashara zangu mwenyewe,” alisema.

Mwandishi wa habari hizi alimuuliza swali msanii huyo, kwamba endapo ataamua kufanya biashara pekee anatafanya ishu gani ambayo itajenga maisha yake alijibu “Zipo biashara nyingi hata saluni naweza kufanya kwa sababu kazi ni kazi hivyo yoyote naweza fanya,”